Stori: Issa Mnally SHEREHE
ya siku ya kuzaliwa ya msanii wa muziki na filamu, Baby Joseph Madaha
‘Baby Madaha’ iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Kijitonyama
jijini Dar es Salaam, ilitawaliwa na vitendo vichafu mwanzo mwisho.
Hafla hiyo iliyohudhuriwa na watu wachache wakiwemo baadhi ya
wasanii, ilifanyika katika Grosari moja iliyopo Kijitonyama.Miongoni mwa
mastaa waliohudhuria alikuwa ni mcheza soka wa zamani wa timu ya Yanga
ya jijini Dar, Samson Mwamanda.
Sherehe hiyo iliyoanza mishale ya saa 6.00 usiku ilitawaliwa na
vituko kibao vilivyowaacha midomo wazi baadhi ya wahudhuriaji.Moja ya
vituko hivyo ni pale Baby Madaha aliyekuwa amekolea kwa kilevi alipoamua
kupigana denda laivu na msanii Isabela Mpanda ambaye naye alikuwa
kachangamka ile mbaya.
Isabela alikuwa kituko zaidi kufuatia kuvaa kinguo kifupi cha pinki
kilichoacha sehemu kubwa ya mwili wake, hasa kuanzia mapajani kuwa wazi.
Msanii huyo pamoja na kujitupa huku na huko kilevi na kucheza muziki
kwa kukata nyonga kinoma, alikuwa akiinua nguo yake juu na kuonesha
kufuli lake ‘white’ na kujishika sehemu za nyuma jambo lililomfanya
mmoja wa wahudhuriaji kusema:
“Jamani pombe ni noma, mnaona mambo ya aibu anayoyafanya Isabela?”
Kituko kingine ni pale mastaa hao waliokuwa bwii kwa kilevi akiwemo
Mwamanda, walipoamua kummwagia pombe kichwani na kwenye nguo zake Baby
Madaha baada ya kumuimbia wimbo wa ‘Happy birth day to you…!’






