IFAHAMU HISTORIA YA DIAMOND PLUTNUMZ NA ROME JONES

Admin Updates10 years ago98 Views


Na Musa Mateja
Kwa
sasa tunapozungumzia mastaa wa muziki wanaofanya vizuri hapa Bongo,
jina la Nasibu Abdul ‘Diamond’ lazima litachukua nafasi ya kwanza kisha
wengine watafuata. Ni kijana anayejituma sana na jitihada zake hizo
zimemfanya awe maarufu barani Afrika.

Picha tofauti wakati wa utoto wao.


Nyuma ya mafanikio ya Diamond
wapo watu wengi. Mwenyewe amekuwa akimshukuru sana mama yake, Sanura
Kassim ‘Sandra’ kwa malezi aliyompa hadi kufikia hapo alipo leo.
Ukimuacha mama yake, wapo watu wengine wengi lakini leo nataka kukupa
angalau kwa uchache uhusiano uliopo kati ya Diamond na DJ wake, Romy
Jones.
Katika safari ya kimuziki, Diamond na Romy wametoka mbali
sana. Kwa wasiojua, wawili hawa ni ndugu kabisa, ni mtu na kaka yake kwa
upande wa mama zao. Yaani mama wa Diamond na mama wa Romy ni mtu na
dada yake.
Mwandishi wa makala haya, alipata nafasi ya kuzungumza na Diamond juu maisha yake na Romy enzi za utoto wao, soma hapa chini…
Maisha ya utotoni
Diamond:
“Awali Romy alikuwa akiishi Kinondoni kwa baba yake lakini kila
wikiendi alikuwa anakuja Tandale, tunakula ‘good time’ kisha anaondoka.
Ikafika kipindi baba yake akafariki na hapo ndipo mama wa Romy
alipolazimika kurudi kwao, Tandale akamkuta dada yake (mama Diamond)
akiwa na mimi. Hapo ndipo tukakua na kucheza pamoja.

“Hakuna
sehemu ambayo ungemkuta Romy bila mimi kuwepo. Yalikuwa ni maisha f’lani
ambayo natamani yajirudie. “Ukweli Romy alikuwa ni mkubwa kwangu lakini
tuliishi kama mapacha licha ya kwamba Romy alikuwa mtundu kuliko mimi.

Nasibu Abdul ‘Diamond’.

Ishu ya shule ikawaje?
Kwa namna tulivyokuwa ilikuwa ngumu kupelekwa shule tofauti, tulisoma shule moja kuanzia shule ya msingi hadi sekondari.

Ubishoo ilikuwa
tangu utotoni
“Unajua
sisi wazazi wetu walikuwa wa kisasa, walikuwa wanajua kutuvalisha
vizuri na ndiyo maana picha nyingi za utotoni cheni, raba, jinzi na
tisheti za kijanja kama kawa. Kwa hiyo huu usafi hatukuuanzia juzi wala
jana, sisi tangu ‘long time’ kitambo.”

Walichopendelea zaidi
“Enzi
hizo tukiwa wadogo hatukujua kama tutakuja kufanya muziki, tulifanya
mambo mengi ya kitoto tu. Tulikuwa tunacheza sana mpira kama ilivyo kwa
watoto wengine.”

Muziki ilikuwaje?
“Wakati tuko wadogo,
nakumbuka kuanzia tukiwa shule ya msingi, mama yangu alikuwa akitupeleka
sana kwenye maeneo ya burudani. Ikitokea kuna mashindano ya kuimba
‘talent show’ alikuwa akitushika mkono na kutupeleka, huko ndiko
tulikoanzia mambo ya muziki.”
Mwanzo wa ustaa


Romy Jones.

Romy
alipokuwa akifanyiwa ‘intaviu’ katika Kipindi cha Sporah hivi karibuni
alisema: “ Wakati nilipoanza kufanya kazi ya utangazaji pale Clouds,
Diamond hakuwa lolote, alikuwa akiniona kwenye TV, yeye bado anapambana
na maisha ya uswahilini huku akifanya muziki.
“Wakati mimi naanza kupata zile elfu 10 na zaidi, yeye alikuwa hana hata mia. Nikawa namtoa kimtindo.
“Ikafika
kipindi ndiyo nikamtambulisha Diamond kwa watangazaji wenzangu akiwemo
Adam Mchomvu, nikawaambia nina mdogo wangu anaitwa Diamond anaimba,
tunamsaidiaje.

“Tukarekodi nyimbo kibao zikaishia hewani. Kuna
moja ya kurap tukafanya na Gez Mabovu na Gwea (wote marehemu) kisha
nikaipeleka Clouds. Mchomvu alipoisikia akaipenda ikaanza kupigwa,
Diamond akawa anafurahi sana. Safari ya kimuziki ikaanzia hapo na mpaka
sasa mimi ni Official DJ na Tour Manager wa Diamond.

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...