CHEKI HII COLLABO YA MAFIKIZOLO, DIAMOND NA MASTAA WENGINE AFRICA… ‘TELL EVERYBODY’ (VIDEO)
10 years ago109 Views
Share
Good news mtu wangu, ile collabo ya kundi la Mafikizolo kutoka South Africa na mtu wetu Diamond Platnumzimetoka!
‘Tell Everybody’ ndio njia la wimbo, na ni wimbo ambao ni sehemu ya project ya Umoja wa Mataifa iitwayo UN Sustainable Development Goals (SDGs) yenye dhamira ya kupambana kutokomeza umasikini, kurekebisha tabia nchi na kuhamasisha usawakufikia mwaka 2030.
Diamond Platnumz.
Wimbo huu umeshirikisha pia wasanii kutoka nchi nyingine za Kiafrika, wapo wakina Yemi Alade kutoka Nigeria,Sauti Sol kutoka Kenya, Toofan kutoka Togo, Becca naSarkodiekutoka Ghana na Diamond Platnumzndiye staa aliyewakilisha +255Tanzaniapamoja na Mafikizolo kutoka South Africa!
Kuna mchanganyiko pia wa lugha mbalimbali ikiwemo Kiingereza, Kifaransa, Kiswahilina Kizulu... kizuri zaidi ni kwamba kila verse utakayoisikia kwenye wimbo huu basi ujue imeandikwa na msanii mwenyewe!
Hapa ninazo baadhi ya picha za wasanii walioshiriki kufanikisha hii project mtu wangu…
Becca Kutoka Ghana
Diamond Platnumz, Tanzania.
Mafikizolo na wasanii wengine.
Diamond Platnumz na wasanii wengine.
Mafikizolo, South Africa.
Nhlanhla Nciza wa Mafikizolo.
Theo wa Mafikizolo.
Yemi Alade, Nigeria.
Kama bado hujabahatika kukutana na video ya ‘Tell Everybody’ karibu uitazame hapa chini…