
MAPENZINI: Swala la mapenzi ni jambo
binafsi, lakini linapokuja kwa watu mastaa huwa lazima lilete stori.Leo
nimetua kwa mwigizaji nguli na mahili wa filamu hapa Bongo, Blandina
Chagula “JOHARI”.
Ni
muda mrefu sasa tangu aachane na aliekuwa mpenzi wake wa siri Vicent
Kigosi “Ray” ambae pia ni mwigizaji na muongozaji wa filamu, mwana dada
Johari kwa mara ya pili sasa ametokelezea akiwa na jamaa mwingine ambae
amezua maswali mengi bila majibu kutoka kwa Johari mwenye.
KIVIPI?
Takribani
miezi kadhaa iliyopita Johari kupitia ukurasa wake kwenye mtandao wa
instagram, aliweka picha hio hapo juu na kuandika “Washa Movie iendelee”
kwa wapenzi wa habari za UBUYU hapa mtakuwa mlimsoma vyema dada yetu.
Hii ilizua mjadala miongoni mwa mashabiki wake huku wengine wakisema
huyu jamaa ndio kachukua nafasi ya kaka yetu Ray wakati wengine wakisema
anafanya hivyo ili kumrusha roho Ray ambae kwa wakati huo penzi lake na
Chuchu Hans ilikuwa jipya na motomoto. Mbali na comment nyingi kumtaka
Johari afunguke, bado Johari alipiga kimya. Mzee wa Ubuyu namimi nikawa
kama vile nimeipotezea movie hii.
Kilichokuja
na kunifanya niikumbuke movie ni hivi majuzi kuweka picha tena akiwa
na jamaa huyo wakiwa kwenye sherehe ya harusi na bila kuandika chochote,
kwamaana nyingine aliwachia mashabiki wajiongeze wenyewe…sasa comment
zaidi ya asilimia 70 zilikuwa zisomeka, Shemejiiii, mnaendanaaa mara
ooh…safi sana…..Ilimradi kila mtu aliandika kile nachojisikia, Johari
hakujibu kitu ila wengi waliamni kuwa hapa kuna jamboo na watu kuwa wapo
penzini.
Namimi mzee wa ubuyu nikaonasiombaya nikuletee hii movie ili nawe uone na uiache iendelee.