Wanawake ndio wanaongoza kwa kulizwa Sana kwenye mahusiano kuliko
wanaume, kwasababu mwanamke akishampata mwanaume aliyekuwa anamtaka basi
atampenda kwa kila kitu, moyo na mwili wake wote kwa haraka wakati yeye
mwanaume hakupi vyote anakuangalia kwanza mpaka atakapoona kweli ndio
kitu anachokitaka ndio ataanza kukupenda kwa ukweli sasa. Lakini akiona
hakuna kitu atakuchukulia poa poa na baadaye anakupotezea, sasa wewe
uliyekufa na kuoza lazima upate ugonjwa wa moyo.
Mwanamke usiende kwenye mahusiano kwa kuangalia picha ya nje, anza
kwanza kumwangalia Kama anaweza kuwa Mume na je unampenda kweli,
ukijihakikishia hapo anza kuwa wife material msaidie mwanaume hata kwa
mawazo tu sio unakaa tu kazi yako wewe ni kuzungusha kiuno tu.
Inatakiwa ukiingia kwenye maisha ya mwanaume mwenyewe anakiri hakuna
mwanamke Kama wewe. Unambadilisha hata Kama hakuwa muoaji ajue umuhimu
wa mke na kutaka kukuoa.