Ijumaa: Mambo ya utangazaji umeachana nayo au una mpango wa kusaka kazi sehemu nyingine?
Penny:
Unajua hakuna kitu kizuri kama mtu kuwa na taaluma yako kichwani, yaani
hata kama nitakaa miaka kumi bado fani yangu itakuwa ni utangazaji.
Ijumaa: Kuna tetesi kuwa ukikasirishwa tu na mpenzi unakimbilia kunywa sumu, ni kweli?
Penny: (kicheko) Hao wanaosema hivyo watakuwa wananijua sana kuliko mama yangu, siko hivyo wanavyodai jamani.
Ijumaa: Mwanaume ambaye uliamua kumuweka wazi alikuwa ni Diamond tu, kwa nini sasa hivi unaficha?
Penny: Unajua kuna mwanaume mwingine hapendi mambo ya kujulikana kwani wote siyo mastaa.
Ijumaa: Kwa sasa wewe na Wema ni marafiki, je mkikaa huwa hamuongelei mambo ya mpenzi wenu aliyepita?
Penny: Hakuna kitu kama hicho, sisi huongelea mambo yetu binafsi kwani urafiki wetu ni tangu kitambo.
Ijumaa: Kuna kipindi ulivalishwa pete ya uchumba na ulikuwa mbioni kuolewa, ilikuwaje?
Penny: Ni kweli na lengo bado liko palepale, ikifika muda nitaolewa kwani sijatangaza kama tumeachana.
Ijumaa: Kuna kipindi ulikutana na mtihani kupitia mitandao ya kijamii, ulijifunza nini?
Penny:
Nilichojifunza ni kwamba watu wengi wanaotumia mitandao ya kijamii
wanakurupuka na hawana utu kwani wanaweza kupoteza uhai wa mtu kama
hayuko imara.
Ijumaa: Ulishafikiria kutoa uhai wako kwa ajili ya mitandao ya jamii?
Penny:
Nilishawahi kuwaza nijiue lakini namshukuru sana mama yangu aliniambia
kuwa hakuna kitu ambacho hakiwezi kuisha hata siku moja.
Ijumaa: Unazungumziaje bifu la Kajala na Wema?
Penny:
Mimi ninachojua wale ni marafiki wanaopendana sana, ipo siku tofauti
zao wataweka pembeni kwa sababu siku hizi hakuna haja ya kuwekeana
mabifu.
Ijumaa: Ulishawahi kwenda kwa mganga kwa kusaka mafanikio au jambo lolote?
Penny:
Siku zote katika maisha yangu mganga wangu ni Mungu maana ananijibu kwa
haraka sana, sijawahi kumtegemea mganga wala hilo halitatokea.