MAHAKAMA YABATILISHA KIFUNGU CHA SHERIA KINACHOWARUHUSU WAKURUGENZI WA HALMASHAURI KUWA WAIMAMIZI WA UCHAGUZI

Special Correspondent6 years ago82 Views

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imebatilisha  kifungu cha sheria cha  7(3)kinachowaruhusu Wakurugenzi wa Manispaa na Halmashauri kuwa wasimamizi wa Uchaguzi nchini. 

 Uamuzi huo umetolewa leo Mei, 2019 Uamuzi his na Jaji Atuganile Ngwala kunatokana na kesi namba 8 ya mwaka 2018 iliyofunguliwa na   Mwanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Bob Chacha Wangwe.

Aidha katika maamuzi hayo Jaji Ngwala,  ametengua kifungu cha 7 (1) kinachoruhusu mtu yeyote kuwa msimamizi wa uchaguzi na kusema kuwa sheria hizo ni batili na kinyume cha katiba ya nchi.

Akisoma uamuzi huo, Jaji Ngwala amesema kwa mujibu wa ushahidi uliowasilishwa kwenye mahakama hiyo na mpeleka maombi kuwa wasimamizi wa chaguzi ni wanachama wa chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao wanamaslahi kwenye chaguzi hizo.

Mpeleka maombi (Bob) katika kesi hiyo amewakilishwa na Wakili Fatma Karume, ambae aliwasilisha ushahidi wa majina74 ya wasimamizi wa uchaguzi ambao ni wanachama wa (CCM). Kama ushahidi wa dhidi ya shauri hilo.

Jaji Ngwala amesema kuwa sheria  hizo hazijaelekeza utaratibu wowote wa kuhakiki kuwa wasimimizi hawana maslahi binafsi na uchaguzi.

Amesema ya Kuwa  sheria hii ya Tume ya Uchaguzi imekataza mtu yoyote ambaye mwanachama wa chama chochote haruhusiwi kuwa msimamizi wa Uchaguzi.

from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2vTfQmo
via

Previous Post

Next Post

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.