DR MSHINDO MSOLLA AMBWAGA DR TIBOROHA KWA KISHINDO

Special Correspondent6 years ago4 Views

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Zoezi la kuhesabu kura za uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Yanga umemalizika na Dr Mshindo Msolla kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga kwa jumla ya kura 1276 katika Uchaguzi uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Msolla amembwaga mpinzani wake Dkt Jonas Tiboroha aliyepata kura 60 huku kura 5 zikiwa zimeharibika.Mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga Fredirick Mwakalebela amefanikiwa kushinda nafasi hiyo baada ya kupata jumla ya kura 1206 kati ya kura 1341.

Mwakalebela amewapiku wenzake wanne ambao wote walikuwa wanawania nafasi hiyo kwa kura nyingi.Wagombea hao Titus Osoro alipata kura 17, Yono Kevela kura 31, Chota kura 12 na Janeth Mbeni akipata kura 61 na kura 21 zikiwa zimeharibika.

 Katika nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji waliochaguliwa ni Hamad Islam 1206, Engineer Mwaseba 1174, Dominick Ikute 1088, Kamugisha Kalokola 1072, Arafat Haji 1024, Salum Ruvila 976,Saad Khimji 788 na Rodgers Gumbo 776

Uchaguzi Mkuu wa Yanga umefanyika leo kwenye ukumbi wa Police Officers Mess Oysterbay na jumla ya wanachama 1341 walijitokeza kupiga kura.
Dr Mshindo Msolla Mwenyekiti mteule wa Klabu ya Yanga

from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2V2zqqr
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...