ZARI AMCHANGANYA BABA YAKE DIAMOND, AMWAGIWA SIFA KIBAO UKWENI..HEBU ONA HAPA

Admin Updates10 years ago8 Views

Kukubali!
Baba mzazi wa mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’,
Abdul Jumaa ‘Baba D’ amefunguka kuwa, kwenye listi ya wanawake wote
waliowahi kuwa na mwanaye kimalovee, mwanadada Zarinah Hassan ‘Zari The
Boss Lady’ ndiye mkwe wa ukweli kwake kutokana na kuwa tayari kumletea
mjukuu.
Mkali
wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mpenzi wake Zarinah
Hassan ‘Zari’.Akizungumza na Amani, juzikati jijini Dar, baba Diamond
alisema kuwa miongoni mwa vitu ambavyo vilikuwa vikimkosesha amani ni
maneno yaliyokuwa yakimsakama Diamond kuwa huenda hana uwezo wa kumpa
mimba mwanamke, kiasi cha warembo wote aliowahi kuripotiwa kutoka nao
kutoka patupu bila kushika ujauzito.
“Nawashangaa
sana hao wanawake si huyo Wema (Sepetu) wala hao wenziye, maana Diamond
alisema kampa mimba Penny (Penniel Mungilwa) zikatoka huku mwenyewe
akikanusha hajawahi kushika mimba kwa kumchafua tu mwanangu aonekane
siyo mwanaume rijali,” alisema mzazi huyo.

Baba
mzazi wa mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Abdul
Jumaa ‘Baba D’.Baba D alitiririka kwamba mastaa hao wa kike ambao Mbongo
Fleva huyo aliwahi kutoka nao huenda wao ndiyo hawana kizazi hivyo
wanamtupia lawama mtoto wake kwa kushindwa kuwazalisha.
Alisema kuwa
kikubwa anachokiamini wote hawakuwa na upendo wa kweli kwa mwanaye,
walitaka kuzitumia tu fedha zake na kumuacha solemba lakini sasa Zari
ndiye mwenye penzi la dhati kwa mwanaye.
“Kiukweli Zari kanifurahisha. Ndiye mkwe wangu wa kweli na halali kabisa.
“Nampongeza sana Zari kwa kushika ujauzito wa mwanangu. Sasa Diamond atatembea kifua mbele kwa kujiamini,” alisema baba D.
Alisema
kutokana na kile kilichokuwa kikiaminika kuwa hana maelewano mazuri na
mkali huyo wa Bongo Fleva, kwa sasa wapo vizuri na hata akiwa na tatizo
huwa anamwambia Diamond ambaye amekuwa akimpa msaada.
“Kwa sasa nina
maelewano mazuri na Diamond, muda wowote nikiwa na tatizo huwa
namjulisha ananisaidia, kitu ambacho kinamfanya amgharamie mama yake
kuliko mimi ni kwa sababu aliishi naye kwa kipindi kirefu na kuhangaika
naye tangu utotoni,” alisema.
Ukiacha Zari ambaye amekubali kubeba
ujauzito wake, Diamond aliwahi kuwalalamikia baadhi ya wapenzi wake kuwa
walikataa kumzalia mtoto akiwemo Wema, Penny na Jokate Mwegelo

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...