RAIS WA ZANZIBAR ALHAJ Dk. Ali Mohamed Shein Atowa Salamu zac Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Special Correspondent6 years ago4 Views

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein amewanasihi wafanyabiashara kuwa waadilifu katika kuwafanyia wanunuzi tahafifu za bei za bidhaa na huduma nyenginezo hasa katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Alhaj Dk. Shein aliyasema hayo katika risala maalum aliyoitoa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari katika kuukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani katika mwaka huu wa 1440 Hijria sawa na mwaka 2019 Miladia.
Katika risala yake hiyo, Alhaj Dk. Shein aliwataka wafanyabiashara kukumbuka kwamba kwa kufanya hivyo hawatokula hasara bali watazidi kupata fadhila mbali mbali za Mola wao Mlezi zinazoambatana na Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Aidha, aliwataka wakulima waendelee na ustaarabu pamoja na utamaduni wao ule ule wa ustahamilivu na uadilifu kwa kujiepusha na tabia ya uvunaji na uuzaji wa mazao machanga.

Rais Dk. Shein aliongeza kuwa lengo la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar si kumkomoa mtu kwa sababu Serikali huwa haiwakomoi wananchi wake bali dhamira yake ni kuwalinda na kuona kwamba hawafikwi na matatizo ambayo yanaweza kuepukika na kujikinga nayo. 

Pamoja na hayo, Alhaj Dk. Shein alitoa nasaha zake kwa wale ambao si Waislamu na wale ambao watakuwa na dharura zinazowazuwia wasifunge kuwa wasifanye vitendo vitakavyoathiri wanaofunga.

Alhaj Dk. Shein alisisitiza haja ya kuhimizana zaidi kuisoma Qur-an kwa wingi ndani ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na kujitahidi kufahamu mantiki ya maelekezo yake.

Aliwataka waumini kuhimizana kuhudhuria darsa katika misikiti ndani ya mwezi wa Ramadhani na kuepuka kutumia muda kwa kufanya mambo yasiyo na manufaa katika mwezi huo ambayo yanapingana na mafunzo ya Uislamu na silka zao.

Sambamba na hayo, Rais Dk. Shein aliwatakia kila la heri Wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi wakiongozwa na Spika Zubeir Ali Maulid katika Mkutano wao wa 14 wa Baraza la Tisa la Wawakilishi utakaojadili Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha wa 2019-2020.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein

from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2PMlIag
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...