MAPENZI:ETI KUMBE HIZI NDIZO SABABU ZA WANAUME KUCHEPUKA??…HEBU SOMA UJUE

Admin Updates10 years ago7 Views


Mambo
vipi msomaji wa safu hii. Bila shaka unaendelea vizuri na harakati zako
za kimapenzi na kwa mara nyingine upo tena katika safu hii ili
kufuatilia nini kimejiri.

Moja
ya tatizo kubwa kabisa linalowasumbua wapenzi wengi ni tabia ya
kutoaminiana baina yao. Kila mmoja hudhani mwenzake anakwenda kinyume na
hili, mara nyingi lawama huenda zaidi kwa wanaume kwani ni wepesi
kuchepuka.


Zifuatazo ni baadhi ya sababu zinazosababisha wanaume kutoka nje ya uhusiano wao wa kimapenzi.



Hulka(Tabia)


Wanaume
wengine wana tabia tu ya kupenda kuwa na wapenzi wengi, hawaridhiki na
mwanamke mmoja. Hawana hofu ya Mungu na hili hulifanya hata kama hakuna
ugomvi wowote nyumbani. Kwao, kile demu aliyependeza anayekatiza mbele
yao wanamtamani.

2.  Kutojiachia faragha


Labda
hili wengi hawapendi kuliweka wazi. Wanawake ni watu wa aibu, hawapendi
kujiachia kwa kuonesha wanachojua chumbani, wanaamini kwa kufanya hivyo
wataonekana wahuni. Kwa sababu hiyo hupenda kushiriki tendo
‘kistaarabu’ na heshima, tena hivyo hivyo kila siku, inachosha. Mwanaume
anaona bora ‘akatesti’ ladha nyingine nje.





3. Mkumbo 



 
   Wanaume wengi hasa hawa vijana wa sasa wanafuata mkumbo wa marafiki
kwa kutaka kufanana nao. Wakiona kila kwenye tukio flani wenzao wamekuja
na ‘vitu vipya’ nao hutamani kuwa hivyo, hivyo kujikuta wakichepuka.
Baadhi yao hujisifu kijinga kuwa hata wazazi wao walikuwa viwembe hivyo
wamerithi.



4. Umaarufu


Baadhi
ya wanaume hudhani kuwa kuchepuka ni sifa inayowapa umaarufu kwa
kuonekana wao ni hodari. Wengine hutaka kuonesha kuwa wao ni vidume vya
mbegu. Ingawa kimsingi inawaondolea heshima kwa kutongoza kila mwanamke
anayekuwa mbele yao, lakini kwao ni fahari ya kujitapa nayo mbele ya
wenzake.



5. Mazingira


Wakati
mwingine wanaume huponzwa na mazingira wanayoishi au anayokuwemo.
Akienda safari, kwa mfano aina ya marafiki na matendo yao wanapokuwa baa
au sehemu ya starehe yanaweza kumgeuza juu ya mwenendo wake, hasa kwa
wanawake. Huogopa kuonekana ‘mshamba’…..
Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...