Mama akamatwa Kwa Kumfungia Mtoto wa Kambo kwa Miaka 20

Admin Updates2 months ago7 Views

 Akamatwa Kwa Kumfungia Mtoto wa Kambo kwa Miaka 20

Mwanamke mmoja kutoka Connecticut, Kimberly Sullivan (56), amekamatwa baada ya kijana anayesemekana kuwa mtoto wake wa kambo kudai kuwa alimfungia ndani ya nyumba kwa zaidi ya miaka 20 na kumtesa. Kijana huyo wa miaka 32 alikiri kwa polisi kwamba aliamua kuwasha moto ndani ya chumba chake ili kupata uhuru wake.

Kwa mujibu wa polisi wa Waterbury, kijana huyo alisema alikuwa akinyanyaswa, kunyimwa chakula, na kutopata huduma za matibabu kwa miaka 20. Aliwaambia wazima moto kuwa, “Nilitaka uhuru wangu,” baada ya kuzima moto huo uliowashwa kwa kutumia sanitizer na karatasi.

Sullivan amefunguliwa mashtaka ya utekaji nyara, unyanyasaji, kumnyima uhuru, na kuhatarisha maisha ya mtu. Wakili wake, Ioannis A. Kaloidis, amekanusha mashtaka hayo, akisema ni madai yasiyo na msingi na kwamba mteja wake hana hatia.

Dhamana ya Sullivan imewekwa kuwa dola 300,000, na atabaki katika mikono ya Idara ya Magereza ya Connecticut akisubiri kesi.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.