Mbunge wa Kigamboni Mhe.Dkt.Faustine Ndungulile
Mwakilishi wa Tanzania katika uchaguzi wa Nafasi ya mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani(WHO) kanda ya Afrika Daktari Faustine Ndugulile,amechaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika hilo la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika katika uchaguzi uliofanyika leo Jumanne, tarehe 27 Agosti 2024 mjini Brazzaville, Jamhuri ya Congo. Dkt. Ndugulile aliyeungwa Mkono na Serikali ya Tanzania pamoja na viongozi wake akiwepo Rais Samia amewashinda kwa kishindo wagombea wengine watatu kutoka Senegal, Niger na Rwanda.