AJALI YA NDEGE YAUA 41, YAJERUHI 11 NCHINI URUSI

Special Correspondent6 years ago39 Views


Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
TAKRIBANI watu 41 wamefariki dunia kufuatia ajali ya ndege ya Aeroflot Sukhoi Superjet ya nchini Urusi baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria kushika moto na kulazimika kutua kwa dharura mjini Moscow hapo jana, shirika la utangazaji la Al jazeera limeripoti.

Video zimeonesha  ndege hiyo ya Sukhoi Superet -100 ilipata hitilafu na kulazimika kutua kwa dharura huku sehemu za ndege hiyo ikiwaka moto katika uwanja wa ndege  wa Sheremetyevo Moscow.

Baadhi ya picha za video zimeonesha baadhi ya abiria wakiruka kutoka katika sehemu zilizokuwa zinawaka na kuruka katika nyasi na sehemu salama.

Imeelezwa kuwa watoto wawili ni moja kati ya watu waliopoteza maisha na tayari wapelelezi kutoka Urusi wameshaanza kufanya uchunguzi kufuatia tukio hilo.

Waziri wa Afya wa Moscow Dmitry Matveyev amesema kuwa katika ajali hiyo watu 11 wamejeruhiwa, na watatu kati yao wameruhusiwa kutoka hospitali na hali zao zinaendelea vizuri.

Mamlaka ya uwanja wa ndege Moscow Urusi umesema kuwa ndege hiyo ilitua kwa dharura baada ya tatizo la kiufundi kutokea ikiwa angani na  wachunguzi watafanya utafiti kupitia mashahidi, wahanga pamoja na wafanyakazi wa ndege wa la shirika hilo.

Ndege hiyo ya Sukhoi  aircraft ilikuwa inaruka kutoka Moscow kuelekea mji wa kaskazini wa Urusi (Murmansk) kabla ya kurudi uwanjani na ilibeba abiria 73 na wafanyakazi wa ndege 4.

from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2PLueX9
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...