Ahamia Haki Elimu
“Baada
ya kucheza filamu nyingi, nikabahatika kuingia kwenye matangazo
mbalimbali na mara ya mwisho niliingia kwenye yale ya Haki Elimu ambapo
nilionekana kama mwanafunzi.
Zaidi ya usanii
“Mbali na masuala ya uigizaji, sasa hivi nafanya biashara mbalimbali.
Ana undugu na Mainda?
“Mainda
siyo ndugu yangu kama baadhi ya watu wanavyofikiri, ni mtu wangu wa
karibu sana ambaye kwenye maisha yangu ya kisanii amechangia kwa kiasi
kikubwa. Ndiyo maana tunaitana mapacha.
Amzungumzia Lulu
“Wengi
wanakumbuka nilivyomsaidia Lulu alipokuwa gerezani na hata baada ya
kutoka nilikaa naye pale kwangu kwa siku kadhaaa. Yule pia ni zaidi ya
rafiki yangu na tumekuwa tukisaidiana kwa mengi.
Ni kweli yeye na Kalala Junior ni wapenzi?
“Naomba
hili nisilizungumzie kwa leo kwani nahisi ni mapema sana. Watu wanaona
tuna ukaribu sana na kila mmoja anahisi kivyake lakini niseme tu kwamba
muda ukifika nitaweka wazi kila kitu.
Kuhusu malezi ya mwanaye
“Nampenda
sana mwanangu Patrick, nipo tayari kufanya lolote zuri kwa ajili yake
na ndiyo maana watu wanasema namlea vibaya, wakumbuke kuwa mwanangu ni
staa hivyo kunyoa viduku, kuvaa kistaa siyo tatizo.
“Ameshacheza
filamu nyingi na kuonekana kwenye matangazo mengi na amesaini mkataba na
kampuni moja ya matangazo ambayo itamlipa dola 1,300 ambazo ni takriban
shilingi milioni mbili. “Nimemnunulia gari aina ya Passo na ameshaanza
kuiendesha. “Mwanangu napenda aje kuwa rubani,” anasema Muna.