Michezo ya UMISSETA 2021 Imezinduliwa rasmi Mkoani Mtwara leo Juni 21 katika uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mgeni rasmi katika uzinduzi huo alikuwa ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Caroline Nombo. Uzinduzi huo umesindikizwa na burudani mujarabu kutoka kwa wasanii Maua Sama na Chege Chigunda ambao walionekana kukonga nyoyo za mamia ya wafunzi waliofika uwanjani hapo!