Wanafunzi 25 wa Sekondari wauawa Kikatili,Jionee hapa

Special Correspondent1 year ago6 Views

 

Takribani Wanafunzi 25 wa Shule ya Sekondari ya Mpondwe Lhubiriha, (zamani Peter Hunter SS), wameuawa kufuatia shambulizi linaloshukiwa kufanywa na wapiganaji wa Allied Democratic Forces – ADF, katika eneo la Kasese, lililopo magharibi mwa mpaka wa nchi ya Uganda na DRC.
Tukio hilo, limetokea baada ya wanamgambo hao kuvamia Shule hiyo ya kutwa na bweni, wakati Wanafunzi hao walipokuwa wamelala na miili yao ilipatikana katika boma la shule, huku wengi wao wakikutwa wamekatwa kwa vitu vyenye ncha kali.
Kufuatia hali hiyo, Jeshi la Polisi Uganda limepeleka vikosi vya kupambana na ugaidi na vikosi maalum katika shule hiyo, huku ikidaiwa kuwa waasi hao wa ADF pia waliwateka nyara wanafunzi kadhaa, kuiba vyakula na vitu mbalimbali, kabla ya kuvuka kurudi DRC.
Mmoja wa watumishi katika shule hiyo, ambaye hakutaka kutaja jina lake amesema wakati wa tukio kulikuwa na Wanafunzi 50 na walionusurika ni watatu pekee, hivyo ikimaanisha kuwa zaidi ya wanafunzi 20 ndio waliotekwa nyara na wanamgambo hao wa ADF.
Hili linakuwa ni tukio la pili, kwa wanamgambo kushambulia eneo la Uganda kutoka DRC katika kipindi cha chini ya mwaka mmoja, kwani Desemba 2022 jeshi la Uganda liliwaua wapiganaji 11 wa ADF baada ya kuingia Uganda kutoka DRC.
Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.