Serikali ya Rais Magufuli kununua ndege kubwa ya mizigo,Soma zaidi hapa

Special Correspondent4 years ago5 Views


Serikali inatarajia kununua ndege kubwa ya mizigo, ili kuokoa gharama na muda wa usafirishaji wa minofu ya samaki kwenda nje ya nchi, zinazowakabili wamiliki wa viwanda vya kusindika minofu hiyo Kanda ya Ziwa.

Ahadi hiyo ya Serikali imetolewa Jijini Mwanza na mkurugenzi wa Shirika la ndege Tanzania (ATCL) Ladslaus Matindi, baada ya kukamilisha ziara ya kutembelea uwanja wa ndege wa Mwanza na viwanda vya kusindika minofu ya samaki vya Nature’s Fish na Omega.

Hatua ya Serikali kutaka kununua ndege hiyo imefuata, kutokana na uhaba wa ndege za usafirishaji wa minofu ya samaki kwenda nje ya nchi, jambo linalosababisha adha ya usafiri kwa wamiliki wa viwanda vya kusindika minofu ya samaki.
Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) Mhandisi Emmanuel Koroso, amesema kutokana na tatizo hilo, Serikali imeanza kufanya mazungumzo na nchi mbalimbali za kigeni, ili kuruhusu usafirishaji wa mizigo kwa kutumia ndege zilizopo.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.