Ngoma
mpya itakayotoka hivi karibuni ambayo Lord Eyez amemshirikisha Ray C
haimaanishi kuwa mastaa hao waliowahi kuwa wapenzi wamerudisha ukaribu
wao.
Kwa mujibu wa Ray C, wimbo huo ulirekodiwa miaka 7 iliyopita.
Ray C amepost picha hii kwenye Instagram na kuitolea maelezo hapo chini
“Mambo
iende kwa wote wanipendao! Naomba tu kuwajulisha kuwa Nimeskia Lord
Eyes anakaribia kuutoa wimbo uitwao Matatizo ambao alinishirikisha!Najua
wengi wanaweza tafsiri vingine lakini Niwambie tu kwamba Huu wimbo
tuliurekodi miaka SABA ILiopita nchini Kenya kipindi tuko pamoja na si
kipindi cha hivi karibuni!Nimeona niongee tu maana naona magazeti
yashaanza Udaku,” ameandika Ray C kwenye Instagram.