Nay wa Mitego akipozi na Mtangazaji wa Kipindi cha Sporah.
STAA wa Bongo Fleva nchini, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amefunguka kuhusu mali zake anazomiliki.
Nay ameyafunguka hayo wakati akihojiwa katika Kipindi cha Sporah kinachoruka kupitia Runinga ya Clouds TV kila Jumanne usiku.

Nay wa Mitego akipozi na Mtangazaji wa Kipindi cha Sporah.
Staa huyo amesema anamiliki nyumba tatu, magari matatu ambayo ni Toyota Prado, Nissani Murano na Toyota Passo.
Mbali ya vitu hivyo pamoja na muziki, pia staa huyo anavitega uchumi
ambavyo vinamuingizia kipato ikiwemo bajaj, saluni na vinginevyo.

Mojawapo ya mijengo ya Nay.
Kwa upande wa mahusiano, Nay amesema kwa
sasa yupo ‘single’ akiwalea watoto wake wawili baada ya kutofautiana na
mpenzi wake wa tatu Siwema na kuamua kumchukua mtoto wake mchanga
anayedai alikuwa hapati malezi bora kutokana na mama yake huyo kuwa bize
na biashara zake.
Nay akipozi jirani ya mojawapo ya ndinga zake.
Nay ameeleza historia ya mahusiano yake
akiweka wazi wapenzi wake watatu ambao amezaa nao watoto akianza na wa
kwanza ambaye alikuwa Mhindi huku wa pili akiwa msanii wa sinema za
Kibongo, Skyner Ally ‘Skaina’ kabla ya kumaliza na Siwema ambaye
wametofautiana hivi karibuni.
Nay wa Mitego akiwa na Siwema.
Nay amesema kwa sasa ana watoto watatu ambao aliwapata na wapenzi wake hao watatu wa zamani na kati ya hao wawili anaishi nao.
Lakini mbali na kusema kwa sasa yupo single, staa huyo hivi karibuni
amekuwa na uhusiano wa karibu sana na mwigizaji wa filamu za Kibongo Shamsa Ford huku wakipiga picha kadhaa za kimahaba na kuziachia mitandaoni.

Nay na Shamsa.
Kuhusu muziki, Nay amefunguka kuwa yeye anafanya muziki biashara
akiangalia soko la muziki linataka nini ili aweze kuendelea kuwa juu.

Nay akiwa na mtoto wake aliyezaa na Skyner.
Mipango yake katika miziki ni pamoja na kufanya kolabo mbalimbali na
mastaa wa nje akiwemo Wizkid na D’banj na wengineo ambapo baadhi yao
tayari amenza kufanya nao kazi.

Nay akiwa na mwanaye aliyezaa na Siwema.
Kwa upande wa hapa Bongo, Nay amesema anatarajia kutoa ngoma nyingine
ambayo amefanya na mkali wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz huku
akiongeza kuwa atafanya pia kolabo na wasanii wa kike ili kuboresha
muziki wake na kuwapa raha mashabiki wake.