Staa huyo aliwahi kukiri kuwa na uhusiano huo na msanii huyo na kwamba
walishaachana kwa amani, ndiyo maana waliweza kuendelea na kampuni yao
ya masuala ya filamu ya Rj Company.
Juzi Johari ameliambia gazeti la Mtanzania kwamba, muda mrefu alikuwa
akisikiliza wanaodai hana uelewano mzuri na Ray kutokana na kuwa na
uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji Chuchu Hans na sasa ameamua kuweka
wazi suala hilo.
“Ni kwa kipindi kirefu sana yamezuka maneno yanayodai mimi na Ray
tulishawahi kuwa wapenzi, kitu ambacho si cha kweli, tena kibaya zaidi
wameongeza kuwa hatuna maelewano mazuri kikazi,” alieleza Johari.
Aliendelea kufafanua: “Sikuwahi kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi kama
wengi wanavyofikiria na kama ningekuwa na uhusiano wa kimapenzi na Ray
na tumeachana, hata kampuni yetu ingeshavunjika kwa kuwa tungekuwa na
chuki, nawaambia hatutegemei kutengana kikazi wala kirafiki,” alisema
Johari