Pamoja na mambo mengine ambayo aliyajibu kwa ufasaha, Gardner
alipoulizwa juu ya habari zinazozungumzwa mtaani kuhusu kuvunjika
uhusiano wake na Jide au Lady Jaydee, aligoma kulizungumzia kwa kigezo
kwamba kipindi hicho kilimhusu yeye tu.
Mwanamuziki wa Bongo fleva kitambo, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’
Mtangazaji huyo alikwenda mbele zaidi kwa kumwambia Salama kwamba
amwite Jaydee kwenye kipindi hicho ili alielezee jambo hilo kwa
undani.Gardner na Jaydee ambao walifunga ndoa mwaka 2005, wamekuwa
wakidaiwa kuwa hawapo pamoja tena huku majukumu ya mtangazaji huyo
ambaye alikuwa meneja wa mwanamuziki huyo yakielea. Kipindi chake
cha Diary of Lady Jaydee kilichokuwa kikisimamiwa na Gardner ambacho
sasa anakiongozwa na ndugu wa msanii ndugu yake aitwaye Wakazi, Jumapili
iliyopita Jidealionekana kwenye harusi ya ndugu yake aitwaye Lameck
Mbibo aka Dabo ambaye pia ni msanii wa Dance Hall akiwa bila mumewe kama
ilivyozoeleka.