“Ninasali sana kwa sasa aisee, mara nyingi nafanya hivyo mara tatu
kwa siku, ninao uwezo wa kukemea mapepo na yakaondoka, hayawezi kukaa
mwilini mwangu,” alisema muigizaji huyo ambaye miaka michache iliyopita,
aliondokewa na mpenzi wake, Steven Kanumba aliyeanguka na kufariki
mbele yake.
Mtabiri mmoja maarufu jijini Dar es Salaam, Maalim Hassan Yahya
Hussein, alisema tatizo kubwa linalomsumbua binti huyo ni jini mauti
ambalo baada ya kumpenda, halitaki kuridhia uhusiano wake wa kimapenzi
na binadamu.“Hapa nimshauri tu, achukue hatua ya matibabu haraka
iwezekanavyo vinginevyo hali hiyo itaendelea, anatakiwa afanye kafara
kwa kuchinja mnyama yoyote ili aondokane na matatizo haya,” alisema.