Bi.Catherine P. Ndossi akichukua na kurejesha fomu ya Kuomba uteuzi wa Kugombea Ubunge kupitia kundi la Viti maalum Mkoa wa Kilimanjaro leo 02/07/2025 Mjini Moshi.
Mjasiriamali na Kada wa Muda Mrefu ambaye alianza safari yake ya Uongozi akiwa Chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM akiwa kama mwanachama na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Tawi la Chuo Hicho Bi Catherine Paulo Ndossi amechukua na Kurejesha Fomu za kuomba kuteuliwa na Chama Caha Mapinduzi kwenye nafasi ya Uwakilishi wa Ubunge (Viti aalum ) Mkoa wa Kilimanjaro.
Kwa wasiomfahamu Catherine Ndosi Hizi hapa ni Taarifa zake za Msingi
Jina Kamili: Catherine Paul Ndosi
Chama: Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Eneo: Mkoa wa Kilimanjaro
Nafasi: Ubunge Viti Maalum (Special Seats – Wajumbe maalum wa bunge wanaotoka kwa makundi kama wanawake, vijana, walemavu…)
Elimu na Utaalamu
Taarifa za umiliki wa cheti cha elimu (sekondari, vyuo vya diploma au degree) bado hazijapatikana kupatikana mtandaoni. Ilakini, mgombea wa viti maalum mara nyingi huja na sifa za kiongozi wa chama au huduma za kijamii.
Itikadi za Siasa na Upendeleo.
Catherine ni mmoja kati ya wanawake wa Mkao wa Kilimanajaro anayeomba kuteuliwa na chama chake cha Mapinduzi kupitia mchakato wa ndani wa CCM.
Catherine amekuwa na historia ya uongozi ndani ya Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) tawi la chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Jijini Dar es salaam Aliposoma masomo ya stashahada ya Uhasibu ambapo kipindi chake alikuwa kiungo muhimu sana kwa cham cha mapinduzi katika tawi la IFM.
Amekuwa akishiriki katika Matukio muhimu ikiwepo mikutano, kampeni, na ujenzi wa chama kwenye ngazi ya mkoa/kata.
Ajenda Kuu ya Bi Catherine ni Nini?
Anasema upande wake anajua na anaamini kiazi ya wabunge wa viti maalum, hasa wanawake, hutegemewa Kuleta sauti maalum kwa maslahi ya wanawake, kazi, elimu na afya.
- Kusimamia haki za jamii zilizo hatarini au machoni mwa umma hasa wanawake na Watoto wa Mkoa wa Kilimanjaro na taifa kwa Ujumla.
- Kuhimiza maendeleo ya miundombinu na huduma muhimu serikalini.
- Anasema Kupitia Kundi la wanawake anaamini kupitia CCM ni chama imara na kinatupa sauti ambayo inaleta nguvu kubwa ya kugusa mahitaji ya wanawake katika jamii na kuwasemea pia nafasi maalum pia hutoa fursa ya kutetea maslahi ya wanawake kwa kiwango cha kitaifa.’Amesema Catherine.
Masama Blog Inampongeza na Inamtakia Kila la Heri mwanamama huyu jasiri na shupavu Catherine Ndossi katika kwa kutia nia na kwenye mchakato huu wa kuomba Uteuzi wa Chama Cha Mapinduzi kwenye nafasi ya Ubunge Viti Maalumu (Wanawake) kupitia Mkoa wa Kilimanjaro.
Recommended Products
-
2025 Summer Rapper Feid Ferxxo Men’s Cotton Fashion Hip-hop T-shirt Casual and Comfortable Short-sleeved T-shirt Street Wear
Affliate products $22.00 -
3 IN 1 Magnetic Folding Wireless Charger Station For IPhone Transparent Fast Charging For IWatch And Airpods
Affliate products -
Grandpa Of Love hoodies Human French Letters Dad Papa Papy Gift Men Clothing hoodies
Affliate products $22.00 -
Sale!
Lenovo D18 Drone 8K Aerial HD Dual-Camera Intelligent Obstacle Avoidance Brushless Power 5G WIFI Screen Remote Control GPS Drone
Affliate products Original price was: $7.99.$7.89Current price is: $7.89. -
Mini Portable Face Cordless Shavers Rechargeable USB Electric Shaver Wet & Dry Painless Small Size Machine Shaving For Men
Affliate products $44.00 -
New Original T75 Bone Conduction Wireless Bluetooth 5.3 Headphones Sports Earphones HiFi Sound Quality Waterproof TWS Headset
Affliate products $3.33






