Mjasiriamali Catherine P. Ndossi achukua Fomu ya Kuwania Ubunge Viti Maalum Mkoa wa Kilimanjaro

Masama BlogKITAIFASIASAMATUKIO1 week ago72 Views

Bi.Catherine P. Ndossi akichukua na kurejesha  fomu ya Kuomba uteuzi wa Kugombea Ubunge kupitia kundi la Viti maalum Mkoa wa Kilimanjaro leo 02/07/2025 Mjini Moshi.

Mjasiriamali na Kada wa Muda Mrefu ambaye alianza safari yake ya Uongozi akiwa Chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM akiwa kama mwanachama na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Tawi la Chuo Hicho Bi Catherine Paulo Ndossi amechukua na Kurejesha Fomu za kuomba kuteuliwa na Chama Caha Mapinduzi kwenye nafasi ya Uwakilishi wa Ubunge (Viti aalum ) Mkoa wa Kilimanjaro.

Kwa wasiomfahamu Catherine Ndosi Hizi hapa ni Taarifa zake za Msingi

Jina Kamili: Catherine Paul Ndosi

Chama: Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Eneo: Mkoa wa Kilimanjaro

Nafasi: Ubunge Viti Maalum (Special Seats – Wajumbe maalum wa bunge wanaotoka kwa makundi kama wanawake, vijana, walemavu…)

Elimu na Utaalamu

Taarifa za umiliki wa cheti cha elimu (sekondari, vyuo vya diploma au degree) bado hazijapatikana kupatikana mtandaoni. Ilakini, mgombea wa viti maalum mara nyingi huja na sifa za kiongozi wa chama au huduma za kijamii.

Itikadi za Siasa na Upendeleo.

Catherine ni mmoja kati ya wanawake wa Mkao wa Kilimanajaro anayeomba kuteuliwa na chama chake cha Mapinduzi kupitia mchakato wa ndani wa CCM.

Catherine amekuwa na historia ya uongozi ndani ya Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) tawi la  chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Jijini Dar es salaam Aliposoma masomo ya stashahada ya Uhasibu ambapo kipindi chake alikuwa kiungo muhimu sana kwa cham cha mapinduzi katika tawi la IFM.

Amekuwa akishiriki katika Matukio muhimu ikiwepo mikutano, kampeni, na ujenzi wa chama kwenye ngazi ya mkoa/kata.

Ajenda Kuu ya Bi Catherine ni Nini?

Anasema upande wake anajua na anaamini kiazi ya wabunge wa viti maalum, hasa wanawake, hutegemewa Kuleta sauti maalum kwa maslahi ya wanawake, kazi, elimu na afya.

  • Kusimamia haki za jamii zilizo hatarini au machoni mwa umma hasa wanawake na Watoto wa Mkoa wa Kilimanjaro na taifa kwa Ujumla.
  • Kuhimiza maendeleo ya miundombinu na huduma muhimu serikalini.
  • Anasema Kupitia Kundi la wanawake  anaamini kupitia  CCM ni chama imara na kinatupa sauti ambayo  inaleta nguvu kubwa ya kugusa mahitaji ya wanawake katika jamii na kuwasemea pia nafasi maalum pia hutoa fursa ya kutetea maslahi ya wanawake kwa kiwango cha kitaifa.’Amesema Catherine.

Masama Blog Inampongeza na Inamtakia Kila la Heri mwanamama huyu jasiri na shupavu Catherine Ndossi katika kwa kutia nia  na kwenye mchakato huu wa kuomba Uteuzi wa Chama Cha Mapinduzi kwenye nafasi ya Ubunge Viti Maalumu (Wanawake) kupitia Mkoa wa Kilimanjaro.

Leave a reply

Previous Post

Next Post

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...