Khadja: Napata changamoto nyingi tu ikiwemo kutongozwa sana na wanaume. Pia baadhi wananikatisha tamaa wakidai eti siwezi kufika mbali wakati najua naweza.
Khadja: Kwani tatizo liko wapi? Kama nikivaa hivyo najihisi niko huru, wewe kinakuuma nini?
Ijumaa: Wewe ni mtu wa aina gani, na je, ikitokea mtu amekuudhi ni kitu gani huwa unakifanya?
Khadja: Mimi ni mcheshi halafu napenda sana utani lakini kuna muda huwa nakuwa na roho mbaya hasa mtu akinikosea.
Khadja: Ni kweli huwa nakunywa pombe ila huwa silewi sana. Huwezi kuamini nikinywa pombe nakuwa mpole.
Ijumaa: Unawezaje kumudu muziki huku ukiwa unalea?
Khadja: Ni ishu ya kujipanga tu, yupo dada ambaye huwa ananisaidia kumlea lakini muda mwingi nikiwa sina shoo, nakuwa na mwanangu.
Khadja: Sijawahi ila huwa natamani kuua kwa maana unakuta mtu anakuudhi kupita maelezo wakati muda huo una ‘stress’ zako.
Khadja: Huwa nasikia tu kwamba wapo mastaa ambao zao ni kuchukua waume za watu lakini mimi sijawahi kuporwa wala kupora.
Khadja: Mtoto wangu ndiyo furaha yangu, kila ninapomuona huwa nafurahi sana.
Ijumaa: Una mpango wa kuingia kwenye ndoa na mwanaume uliyezaa naye?
Ijumaa: Wewe ni mrembo, unawezaje kukabiliana na wanaume wakware?
Khadja: Mimi ni mrembo ndiyo ila kitu ninachokifanya ni kutowapa nafasi watu wa aina hiyo.




































