Uhusiano kati ya Davido na Diamond Platnumz ulishavunjika siku nyingi
kufuatia issue iliyotokea mwaka jana kwenye fainali za shindano la Big
Brother Africa.
Davido na Diamond Platnumz akiwa studio mwishoni mwa mwaka juzi
Tukio hilo lilimfanya Davido aandike mfululizo wa tweets za mafumbo
ambazo wengi waliamini kuwa ni madongo kwa Diamond aliyewahi
kumshirikisha kwenye remix ya Number One iliyotokea kuwa hit namba moja
Afrika miaka katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.
Kambi ya Diamond ilisisitiza kuwa hakuna ugomvi kati ya mastaa hao
wawili na hata staa huyo wa ‘Nasema Nawe’ hivi karibuni aliwahi kuupa
shavu wimbo mpya Davido kwenye Instagram.
Lakini vipi kama kweli Davido na Diamond bado ni washkaji? Kwa kile
alichokipost Davido kwenye ukurasa wake wa Facebook, huenda wawili hao
wakawa wanaendelea kupanga kufanya makubwa baadaye.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Davido amepost picha ya zamani
akiwa na Diamond kwenye studio yake nchini Nigeria. Kwenye picha hiyo,
Davido ameandika: I think I just recorded a sweeter love song than AYE
.. Hmm this album yo.”
~Bongo5