Baraka da Prince Afunguka Kuhusu Yeye na Linah Baada ya Picha hizi Tata Kuzagaa Mtandaoni

9 years ago91 Views

Msanii Baraka da Prince amekanusha vikali kumshika msanii wa kike wa bongo fleva sehemu za kifuani, na kusema aliyepiga picha hiyo aliikuza.

Akiongea kwenye eNews ya East Africa TV, Baraka amesema hajawahi kufanya kitendo kama hicho kwani walikuwa sehemu yenye watu wengi, na pia hajawahi kuwaza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Linah.

“Siwezi kufanya kitu kama hicho kwa sababu pale pana watu wengi, ile picha ilikuwa ya kawaida, yule aliyeipiga na kuipost amekuwa kama kaikuza, sijawahi kufikiria hata kutoka naye”, alisema Baraka.

Pia Baraka amesema siku ya tukio ambayo ilikuwa ni siku ya kuadhimisha miaka 10 ya muziki wa Christian Bella, aliondoka mapema na hakufanya tukio lolote baya.

“Nimetoka kuperfom nikaondoka zangu, sikukaa hata nusu saa, nimemaliza nikaondoka, wasiwe wanaamini mambo ya hivyo”, alisema Baraka.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.