Katika kuhakikisha malengo hayo yanafikiwa,Katibu mkuu wizara ya elimu sayansi na teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo anatumia kumbukizi ya miaka kumi na sita ya kifo cha hayati Edward Moringe Sokoine kukiagiza chuo kikuu cha Sokoine (SUA ) kuhakikisha kinatumia wataalamu wake katika kufanikisha dhana hiyo.
“kwa pamoja tunakazi kubwa ya kufanya ili kufikia lengo hili kilimo chetu kinapaswa kukuzwa na kuwa cha kisasa Zaidi” alisema dkt akwilapo. Pia katibu mkuu amehaidi kutoa million 750 kutoka mradi wa kukuza ujuzi na stadi za kazi kwa ajili ya kuboresha kalakala ya idara uhandisi kilimo katika chuo hicho cha kilimo SUA..
Kwa upande wake makamu mkuu wa chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Profesa Raphael Chibunda amesema chuo kimeaandaa mdahalo kwa kuwakutanisha wanasanyansi na watu ambao wamefanya kazi pamoja na Sokoine ili kupata kwa kiina yale aliyofanya Marehemu huyo ambapo mada kuu ni Uzalishaji wa kilimo na Viwanda na Maendeleo ya Tanzania mabo ya kujifunza kutoka kwa sokoine na na siku zijazo..
“Tumewaalika wazee waliofanya kazi na hayati sokoine enzi za uhai wake na wametukubalia ambao watatupatia uzoefu wa namna ya utendaji wake enzi za uhai wake jambo litakalokuwa na tija kwetu” alisema Prof chibunda.. mwakilishi wa familia ya aliyekuwa waziri mkuu wa serikali ya awamu ya kwanza hayati Edward Moringe Sokoine Bw. Ole Edward amesema kama familia wameanda wakfu ili kuendelea kuyaenzi yale aliyofanya marehemu Sokoine…
Hayati Edward Moringe Sokoine alifariki aprili 12 mwaka 1984 katika eneo la Wami sokoine wilayani Mvomero akitokae Bungeni katika majukumu ya kikazi na wiki ya kumbukikizi hiyo imeanza aprili 9 mwaka huu na inatarajiwa kufikia kilele aprili 12 mwaka huu na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Raisi mama samia Suluhu Hassani.
from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2VAsL88
via