Acha kabisa! Habari ya mjini
katika ulimwengu wa mastaa wa Kibongo ni madai ya Mbongo-Fleva, Omary
Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ kuwachanganya kimalovee, mastaa wenzake,
Jokate Mwengelo ‘Kidoti’ na Vanessa Mdee ‘Van V’ au V-Money
Chanzo makini kilisema Jokate na
Vanesa kwa sasa ni kama chui na paka kufuatia hivi karibuni Jokate
kudaiwa kuingilia penzi la mwanzake na mpaka sasa eti ndiye
aliyeshikilia usukani.
“Sasa hivi Jokate na Ommy ni mahaba niue kwani mara nyingi wanakuwa pamoja.
“Hadi Jokate anakwenda geto kwa
Ommy jambo ambalo limesababisha yeye na V-Money kutoelewana kwani awali
ndiye alikuwa kiburudisho cha Ommy,” kilidai chanzo hicho.
Baada ya kuzinyaka habari hizi, mwanahabari wetu alimtafuta mhusika mkuu Ommy Dimpoz ambaye alikuwa na haya ya kusema:
“Ehee! Ndiyo nasikia kwako,
kwani wasanii haturuhusiwi kupendana jamani, hata Mwalimu Nyerere (Baba
wa Taifa) alisema tuwe pamoja kwa hiyo Jokate ni rafiki yangu wa karibu
na huyo Vanessa sijawahi kuwa na uhusiano naye but (lakini) alikuwa
mshikaji tu.”
Juhudi za kuwapata Jokate na
Vanessa ziligonga mwamba baada ya simu zao kuita bila kupokelewa hivyo
jitihada zinaendelea ili kila mmoja aeleze la moyoni mwake.Juzikati
picha za Jokate na Ommy wakiwa kimahaba zilizagaa kwenye mitandao
mbalimbali hali iliyozua viulizo kibao kwa mashabiki wao.