Chris Brown amekuwa na kawaida ya kuachana na kurudiana na mpenzi wake
Karrueche,lakini kwa hali ya sasa inaaminika uhusiano huo umevunjika
kabisa. Wawili hao kila mmoja kwa wakati wake wameweka picha na
mfululizo wa maneno katika mitandao kupitia kurasa zao wakibainisha kuwa
kila mmoja yuko singo.
Kwa mujibu wa gazeti la Complex,Chris Brown kupitia tamasha la Cali
Christmas lilifanyika ijumaa amekili kuwa hayuko kwenye mahusiano na
yeyote
Chris Brown na Karrueche wamekuwa katika mahusiano kwa muda wa miaka
minne ambapo wamekuwa wakiachana na kurudiana katika kipindi chote hicho
na ndani ya kipindi chote hicho Chris brown amewahi pia kuwa na
Rihana,kisha tena kurudiana na Karrueche.
Hivi karibuni katika mahojiano ya Radio Hot 97 kwnye kipindi cha Ebro
In The Morning, msanii huyo alizungumzia kuhusu uhusiano wake na
Karrueche,alionekana kumsifia kwa kutamka maneno haya.
‘It’s been almost five years. She’s straight. I dig her man. She’s dope…,’ alisema.
‘I feel like, especially being in this industry, you just need somebody
that understands you; who understands who you are personally except for
your name.
‘Me and her have a real connection, like best friends on top of our
intimacy. At the end of the day, me and her have a great relationship.
We’re best friends.’
Kwa
upande mwingine Chris ameweka picha instagram ikimuonyesha akiwa
amejiachia na Khloe Kardashian na dada zake Kendall na Kylie Jenner.