STAA anayefanya vizuri kwenye tasnia ya filamu Bongo, Aunt Ezekiel
amefunguka kuwa anatamani aone mastaa wawili ambao wana bifu kali, Wema
Sepetu na Kajala Masanja wanamaliza tofauti zao kwani maisha ni mafupi.
Wema na Kajala enzi wakiwa bado mashosti.
Akizungumza na gazeti hili, Aunt alisema kati ya mabifu ambayo angependa
yaishe ni la Wema na Kajala kwani wapo wasanii wamefariki dunia wakiwa
na bifu huku wale waliobaki ambao walikuwa na mabifu nao wakitamani
waamke walau mara moja wamalize tofauti zao lakini haikuwezekana.
“Jamani maisha haya ni mafupi sana na tunatakiwa kujifunza kutoka kwa
wenzetu tuliokuwa nao lakini sasa hivi hawapo tena, natamani sana Wema
na Kajala wamalize tofauti zao kwani ipo siku watakuja kujuta siku
ambayo mmoja wao atakapokuwa hayupo japo siwaombei ila hilo ndilo
tamanio langu kuwaona wakizungumza,” alisema Aunt.