MVUA KUBWA KUNYESHA DAR, RC MAKONDA ATOA RAI

7 years ago108 Views

Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
BAADA ya Mamlaka ya hali ya hewa nchini kutoa tahadhari juu ya mvua kubwa inayotarajiwa kunyesha hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam  Paul Makonda amewataka wananchi kuanza kuchukuwa tahadhari  mapema katika kukabiliana na majanga ya mafuriko huku akiwataka wakazi wa mabondeni na walioko pembezoni mwa mito kuhama katika maeneo hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Makonda amesema kuwa ujenzi holela na tabia ya watu kutupa taka kwenye mifereji inayopitisha maji ya mvua  na mito ndio  chanzo kikubwa cha mafuriko hivyo amewahimiza wananchi kuacha mara moja tabia hiyo huku akiwataka wananchi kumripoti kwa wenyeviti wa mtaa kwa yeyote atakayekaidi hilo.

Aidha  Makonda ametoa siku saba kwa wakala wa barabara za Mjini na Vijijini (TARURA) kuhakikisha wanaziba viraka katika barabara kwakuwa vimekuwa usumbufu na kero kwa watumiaji wa barabara huku akiwaagiza TANROAD kusafisha miundombinu ya Mito,mitaro na madaraja yaliyoziba kwa usalama zaidi.

from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2TCVI5o
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.