Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry William Silaa (Mb.), alipowasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha leo tarehe 12 Machi, 2025 kabla ya kuanza ziara ya siku mbili mkoani humo.
Waziri Silaa alipokelewa na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Makonda, na kumjulisha kuwa yuko mkoani humo kwa ajili ya kutembelea na kuzungumza na vijana wa bunifu changa za TEHAMA (Startups).