Kambaulaya ambaye ni shabiki wa Simba na Manchester City alisema kuwa hakuwa na wasiwasi mara baada ya kupigiwa simu na Meneja Masoko wa Kampuni ya M-Bet, Allen Mushi kuwa ni mshindi wa fedha hizo.
“Niliamini kuwa ni mshindi kwani mimi siyo mtu wa kwanza kushinda droo ya Perfect 12 ya M-Bet kutoka mkoa wa iringa, kuna mwanafunzi alishinda na kupatiwa fedha zake,
“Niamini M-Bet kwa kuwa na washindi wa uhakika katika michezo yao, ndiyo maana nilicheza ‘mikeka’ saba, mmoja nikipatia mechi tisa na mwingine mechi 12,” alisema Kambaulaya. Alisema kuwa kiasi cha fedha alichoshinda ni kikubwa sana na anatakiwa kutuliza akili ili kujua nini anafanya kwa upande wa maendeleo.
“Nimeshinda zawadi ya kwanza, lakini nimeumia sana na matokeo kati ya timu yangu, Manchester City ilipofungwa na Liverpool, niliweka Manchester kuwa ni washindi, hata hivyo alifungwa mchezo huo. Meneja Masoko wa M-Bet Tanzania, Allen Mushi alisema kuwa Kambaulaya ambaye ni afisa polisi mkoani Iringa ataweza kubadili maisha yake kupitia mchezo wao wa Perfect 12.
Mushi alisema kuwa M-Bet itaendelea kuwa nyumba ya mabingwa ambao wamefaidika na msemu huo tokea kuanza kwa ubashiri. “Tumetoa washindi wengi mpaka sasa ambao wamejishindia mamilioni ya fedha na kuweza kubadili maisha yao ya kila siku,” alisema Mushi.
from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2OqIkNn
via