Staa wa Bongo Movies, Jacqueline Wolper, amewaweka njia panda mashabiki
wake kwa kauli yake kwamba msichana aliyekwenye uhusiano wa kimapenzi na
msanii wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’
ameshafahamika, tofauti na alivyokuwa akihisiwa yeye.
“Watu hawana dogo, ukiwa karibu na mtu basi utaambiwa mpenzi wako, Nay
hakuwahi kuwa mpenzi wangu kwa kuwa ni zaidi ya rafiki kwangu, ila watu
wasio waelewa ndiyo walikuwa wakivumisha kwamba tuna uhusiano kwa
maslahi yao, lakini sasa ukweli umejulikana kama mnavyoona na
mnavyosikia Nay ni wa nani,” alieleza Jacqueline bia kumtaja anayetoka
na mwana hip hop huyo.
Wolper aliongeza kwamba taarifa hizo ziliposambaa alipata tabu ambapo
alikuwa akitumia muda mwingi kujieleza kwa watu wake wa karibu kutokana
na tuhuma hizo.
Gazeti la Mtanzania