Simba Watamba Kuifunga Al Ahly, Kocha Awawekea Mtego Uwanja Wa Mkapa

Admin Updates1 year ago5 Views

 KOCHA Mkuu wa Simba, Mbrazili, Roberto Oliveira ‘Robertinho’ amesema hana hofu ya kukutana na Al Ahly ya Misri, kwani anazijua mbinu zote wanazotumia.

Timu hizo zinatarajiwa kukutana katika mchezo wa kwanza wa CAF African Football League unaotarajiwa kucheza Oktoba 20, mwaka huu.

Mchezo huo wa robo fainali ya kwanza unatarajiwa kupigwa Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam kabla ya kwenda kurudiana Misri.

Roberto Oliveira ‘Robertinho

Akizungumza na Spoti Xtra, Robertino alisema kuwa mara baada ya droo ya michuano hiyo kuchezeshwa na wao kukutana na Al Ahly, haraka alianza kuwafuatilia kwa karibu wapinzani wao hao.

Robertino alisema amewafuatilia kwa kupitia video za michezo ambayo wameicheza msimu huu kwa lengo la kuwafahamu wachezaji hatari, hivyo tayari amewafahamu.

“Wapinzani wetu Al Ahly wana wachezaji wengine wazuri na hatari wa kuchungwa, lakini hiyo hainifanyi niwaogope, kwani na sisi tuna wachezaji wakubwa na hatari,” alisema Robertinho.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.