Ajali Mbaya Mbeya, Watu 28 Wamefariki Dunia
Watu 28 wamefariki dunia na wengine tisa wamejeruhiwa mkoani Mbeya kwenye ajali ya barabarani iliyohusisha lori lenye shehena ya unga lililogonga magari mawili kwenye Mteremko wa Mlima Iwambi katika Barabara Kuu ya Tanzania na Zambia (TANZAM) usiku wa kuamkia leo Juni 8, 2025.
Ajali hiyo imetokea Juni 7, 2025 majira ya saa mbili usiku, katika eneo la mteremko wa Mbalizi, mkoani Mbeya baada ya lori hilo kufeli breki na kugonga magari mawili yaliyokuwa mbele yake daladala ya abiria na kirikuu (gari dogo la mizigo).https://www.youtube.com/embed/AW3Ch17IDRU
Kufuatia mgongano huo, daladala hiyo iliingia korongoni na baadaye lori hilo liliangukia juu yake, na kusababisha vifo vya abiria waliokuwemo ndani.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa majeruhi tisa wanapatiwa matibabu katika Hospitali ya Teule ya lfisi…Soma zidi hapa