Serikali yazitaka Muhimbili na Mnazi Mmoja kudumisha ushirikiano

Special Correspondent6 years ago4 Views

Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mh. Harusi Suleiman amezitaka Hospitali ya Taifa Muhimbili-MNH- na Mnazi Mmoja kudumisha uhusiano na ushirikiano uliopo ili kuwaenzi waasisi wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Naibu Waziri Suleiman ametoa kauli hiyo katika hafla ya kuhitimisha tamasha la Pasaka   2019 lililofanyika Visiwani Zanzibar na kuhusisha timu za michezo za Muhimbili pamoja na Hospitali ya Mnazi Mmoja iliyopo visiwani humo.

Akizungumza katika hafla hiyo amesisitiza kwamba timu hizo zimekuwa zikikutaka kila mwaka kwa lengo la kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya pande hizo mbili ambapo mwaka jana tamasha hilo lilifanyika Tanzania Bara. “Ndugu zangu tumefarijika kuja kututembelea katika pasaka hii tunaomba ushirikiano huu uendelezwe kwa faida ya pande zote mbili, pia kikubwa nilichofurahishwa kutoka kwenu ni nidhamu pamoja na maadili kwani hata katika michezo tunasisitiza nidhamu na maadili hakika mnastahili pongezi”. Amesema Naibu Waziri wa Afya Zanzibar.

“Lakini pia yapaswa kuwashukuru viongozi wetu ambao walianzisha muungano wetu ambao umetuwezesha kushirikiana katika nyanja mbalimbali ikiwemo michezo hivyo hatuna budi kuwaenzi kwa kuendeleza na kuiboresha zaidi michezo hii ambayo ilianzishwa mwaka 1972”. Amesisitiza Mh. Suleiman.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi kutoka Muhimbili Dkt. Praxeda Ogweyo, amewapongeza wanamichezo wote walioshiriki katika tamasha la Pasaka 2019 na kueleza kuwa Hospitali ya Taifa Muhimbili ipo mstari wa mbele katika kuhakikisha michezo inaendelezwa katika taasisi hiyo na kutoa fursa kwa watumishi wengi kushiriki.
Naibu Waziri wa Afya Mh. Harusi Suleiman akizungumza na wanamichezo katika hafla ya ufungaji wa tamasha la pasaka liliofanyika Zanzibar na kuhusisha timu za Hospitali ya Taifa Muhimbili na Hospitali ya Mnazi Mmoja.
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi Dkt. Praxeda Ogweyo, akitoa neno la shukrani wakati wa kufunga tamasha hilo.
Baadhi ya wanamichezo wakikiliza neno kutoka kwa Naibu waziri wa Afya.

from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2ILpMWV
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.