Ileje, 10 Juni 2025 – Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mheshimiwa Daniel Chongolo, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Ileje kwa kupata hati safi kutoka kwa Mkaguzi wa Hesabu za Serikali.
Mhe. Chongolo alitoa pongezi hizo leo tarehe 10 Juni 2025, wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika kwa ajili ya kujadili hoja za Mkaguzi.
hicho kilihusisha wajumbe wa Baraza la Madiwani, wataalamu wa Halmashauri, pamoja na wajumbe wa Kamati ya Usalama kutoka ngazi ya Mkoa na Halmashauri.
wa Mkoa aliipongeza Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa rasilimali za umma na uwajibikaji, akisema kuwa hatua hiyo ni kielelezo cha uwazi na uadilifu katika utendaji kazi wa Serikali za Mitaa.
Aidha, aliwataka viongozi na watendaji wa Halmashauri ya Ileje kuendelea kushikilia viwango vya juu vya uwajibikaji na kuhakikisha kuwa mapendekezo yote yaliyotolewa na Mkaguzi yanatekelezwa kwa wakati.
Kwa upande wao, madiwani na viongozi wa Halmashauri walimshukuru Mkuu wa Mkoa na usimamizi makini, na kuahidi kuendelea kushirikiana kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wa Ileje.