Rais Samia Afunguka Mazito kwa Uchungu,Asema “Natukanwa SIJIBU Nimejigeuza Chura”

Admin Updates12 months ago5 Views

 Rais Samia Afunguka "Natukanwa SIJIBU Nimejigeuza Chura"

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu amesema anayasikia matusi anayotukanwa lakini amejigeuza chura anajifanya hasikii na wala hatojibu bali anachotaka yeye ni mageuzi ya kiuchumi ili kuipeleka Nchi ya Tanzania mbele.
Akiongea leo June 11,2024 wakati wa akipokea gawio na michango kutoka Mashirika na Taasisi za Umma Ikulu Jijini Dar es salaam, Rais Samia amesema “Kwenye mageuzi haya Mchechu na Waziri wako lazima muwe unpopular, sijawahi kusikia Waziri wa Fedha akasifiwa hata siku moja, siku zote Waziri wa Fedha analaaniwa, kwahiyo Mchechu na wewe utalaaniwa tu hapa, na nyingine zitakuja personal nyingine kikazi lakini hii ndio kazi niliyokupa simama na ifanye”
“Mimi kazi mliyonipa nasimama na naifanya, na mnashuhudia matusi ninayotukanwa ‘Mpuuzi, hana maana, huyu Bibi , eeh eeh ana hivi!’ mambo tele lakini najigeuza chura kelele zinapigwa nyingi wakiona haujibu wanasema sasa tulitukane litajibu au lijibu, sijibu najigeuza chura masikio sisikii kabisa ninachotaka mageuzi ya kiuchumi ndani ya Nchi hii, anayetaka kunikere anikanyagie uchumi wangu”

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.