Imelda Mtema
STAA wa
filamu Bongo, Wema Sepetu na Mtangazaji Penniel Mwingila ‘Penny’ ambao
wote kwa nyakati tofauti wamewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na
mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ baada ya kuona habari za
mwenza wao huyo wa zamani akiwa na mpenziwe mpya, Zali zinapamba moto
kila siku, wameibuka na kudai hawababaishwi nazo, kwani hivi sasa
wameamua kuingia kazini kwa kufanya bonge la project.
Akizungumza kwa niaba ya mwenzake, Penny alisema kelele za kila siku
wamezichoka na baada ya kukaa pamoja, wameona hiki ni kipindi cha kupiga
kazi badala ya kupoteza muda.
“Tumeamua kuandaa filamu yetu ya pamoja ambayo ninaamini itakuwa ni kali
na ya aina yake. Tumepoteza muda mwingi na hivi sasa tunahitaji kufanya
kazi, tunachowaomba mashabiki wakae tayari kutupokea na hatutaki tena
kushabikia mambo ya Zali na Diamond kwa sababu hayatuhusu,” alisema.