Mwanaume Aliyejitekeza Kwa Moto Kisa Ugumu wa Maisha Kenya Afariki Dunia

Admin Updates1 year ago4 Views

Mwanamume aliyejulikana kwa jina Robert Gituhu aliyejiteketeza kwa moto Siku ya Jana (Alhamisi) akilalamikia ugumu wa maisha alifariki saa Nne na Dakika 20 Usiku wa Jana alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali Kuu ya Pwani, Coast General nchini Kenya.

Msimamizi Mkuu wa Coast General Iqbal Khandwalla amethibitisha kwamba mwanamume huyo aliyekuwa na umri wa miaka 27 alipata asilimia 80 ya majeraha ya moto na kwamba alifariki siku iyo hiyo aliyolazwa hospitalini.
“Madaktari wetu walifanya kila wawezalo, tulimpa dawa na matibabu mengine yaliyofaa, lakini kwa bahati mbaya alifariki saa nne na dakika 20 usiku,’ amesema Bw Khandwalla.
Kwenye video iliyosambazwa mtandaoni mwanamume huyo alionekana akiwa amebeba bendera ya Kenya kabla ya kujiwashia moto katika eneo la Mwembe Tayari, Kaunti ya Mombasa.
Marehemu alikuwa mhitimu wa Chuo Kikuu cha Nairobi. Alisomea taaluma ya uhandisi ambapo alihitimu mwaka 2021.
Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.