Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Daniel Chongolo akimtengeneza kola ya shati mwanafunzi wa shule ya Msingi Kanga wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua kiradi ya maendeleo katika Wilaya ya Songwe.
. Chongolo ambaye ameambatana Kamati ya Usalama ya Mkoa na Sekretarieti ya Mkoa wa Songwe ameanza ziara hiyo leo Jumatatu Agosti 19, 2024, ambapo mradi wa kwanza wa utunzaji wa mazingira katika Kata ya Ifwenkenya alianza saa 11:00 alfajiri.
Katika ziara yake Mhe. Chongolo amekagua ujenzi wa bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika Shule ya Msingi Kanga pamoja na mradi wa maji wa maji wa Gaula-Ilasilo-Kanga-Tete.
Mkuu wa Mkoa na ujumbe wake wamepokelewa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Songwe, ndugu Godfrey Kawacha, Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kamati ya Usalama ya Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, CPA. Cecilia Kavishe, wakuu wa taasisi za Serikali za Wilaya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo qa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe