UKARIBU
wa mastaa wa filamu za Kibongo, Kulwa Kikumba maarufu kama Dude na
msanii mwenzake Ester Kiama unaonyesha kama kuna kitu kati yao baada ya
kuonekana kuwa karibu kwa muda mwingi kiasi kinachotia shaka!
Chanzo
kilicho karibu na wawili hao kimesema mara kwa mara wanaonekana kuwa
karibu kila wanapokwenda na kuonyesha dalili zote za kimahaba, lakini
wenyewe wanadai ni washkaji walio kazini.
Gazeti
hili lilibahatika kuwafuma wakiwa pamoja na walipoulizwa juu ya tuhuma
za kujihusisha kimapenzi, kila mmoja alimtupia msalaba wa kujibu
mwenzake. “Mh, jibu wewe, mimi najua Dude ni kaka yangu na ni
mfanyakazi mwenzangu”, alisema Ester.