Siku
chache baada ya kumwagwa na Wema Isaac Sepetu ‘Beautful Onyinye’,
Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amenaswa kwenye mahaba
mazito na msanii, mtangazaji, mjasiriamali, tajiri na mrembo mkali
kuliko wote Afrika Mashariki, Zarinah Hassan a.k.a Zari au Boss Lady.
Mbongo
Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akimhagi msanii mrembo mkali
kuliko wote Afrika Mashariki, Zarinah Hassan a.k.a Zari au Boss Lady.
HABARI YA TAUNI
Habari
ya ‘mujini’ ilidai kwamba, mahaba ya wawili hao yalianzia safarini
walipokutana kwenye ndege moja wiki iliyopita ambapo Diamond alikuwa
akitokea nchini Nigeria kupitia Afrika Kusini kisha Dar huku Zari
akitokea Afrika Kusini kuelekea Dar kibiashara.
Kwa
mujibu wa chanzo makini, mastaa hao walipokutana kwenye ndege
waliungana na kupiga picha za pamoja kisha safari yao ya mahaba niue
ikaanzia hapo