
NAHODHA wa Stars na straika wa Fenerbahce, Mbwana Samatta yupo mbioni kujiunga na PAOK inayoshiriki Ligi Kuu nchini Ugiriki.
Taarifa za Uturuki zinaeleza tayari Samatta ameshafanya makubaliano na PAOK, anatarajiwa muda wowote kwenda Ugiriki kufanya vipimo vya afya na kusaini.