Wale mafahali wawili waliowahi kutengeneza uzi mrefu humu mwanzoni mwa
miezi February, Mjasiriamali William Malechela Le Mutuz na Mwanasheria
Alberto Msando, kufuatia promoshen iliyotamba ya kampuni ya Coka cola
yenye jina “share a coke” ya kuandika majina katika makopo, hatimaye
wamepatana.
Katika kurasa zao za insta wametupia picha wakiwa pamoja huku wamefunga
mikono style anayoipenda sana mkuu Le Big Show AKA Akili kubwa, huku
kila mmoja akitupia ujumbe kuonesha yameisha.
Ikumbukwe kuwa wakati wa tifu hilo hata wachangiaji wengi humu
walijikuta wakiwa makundi tofauti kila mmoja akiwa upande wa aliyeona
ana hoja ya msingi katika suala lile.
Binafsi mimi nimewapongeza sana hawa jamaa kwa kuonesha ukomavu wa
busara na wito wangu wooote mliokwaruzana kipindi kile tafadhali
rejeaneni.
Alberto Msando Ameandika hivi:
“In life there is only one thing that is permanent. Interests. Live at
the Stars Meeting Millennium Tower. We met! We spoke!! We are so done!!
We are brothers!”