- Home
-
- MAPENZI:YAMENIKUTA: MCHUMBA WANGU AMEZAA ANGALI BADO BIKIRA
MAPENZI:YAMENIKUTA: MCHUMBA WANGU AMEZAA ANGALI BADO BIKIRA
Wanajamvi
habari zenu. Mimi nina mchumba wangu ambaye ni mkristo mwenye imani
sana na dini yake. Mtaratibu, mpole, na ana heshima sana. Katika
mahusiano yetu hatujawahi kufanya mapenzi mpaka tutakapofunga harusi na
pia ni bikra. Nilipata safari kwa mda nimerudi nimemkuta amejifungua
mtoto wa kiume. Nimeshangaa namuuliza kulikoni, anadai mimba hiyo
alipewa na malaika.
Nimemwamini
ila nikamuambia kama ndivyo basi huyu mtoto atakuwa nabii hivyo
amsimamishe ili atembee juu ya maji kama Yesu, akaniambia amefunuliwa
ndotoni kuwa mtoto huyo ataanza kufanya maajabu atakapofikisha miaka
mitano.
Hapa nimeanza kupata shaka naombeni ushauri!
0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)
Stay Informed With the Latest & Most Important News