MAKAVU LIVE:HAWA WASANII‭ ‬WA BONGO‭ ‬MOVIES NI NANI ALIYEWAROGA‭?‬

10 years ago108 Views

KWENU
wasanii wa Bongo Movies‭. ‬Bila shaka mko poa na mnaendelea na
mishemishe zenu za mjini kama kawaida‭. ‬Kutokana na ubize wa kazi zenu
na zangu‭, ‬leo nimeona bora niwakumbuke kwa barua‭.‬

Mkitaka kujua hali yangu‭, ‬mimi ni
mzima wa afya namshukuru Mungu naendelea na majukumu yangu kama kawaida
ambapo moja ya majukumu hayo‭, ‬ni hili la kuwaandikia barua
kuwakumbusha pale ninapoona hamuendi sawa au kuwapongeza mnapofanya
vizuri‭.‬
Dhumuni la barua hii ni kutaka kuwauliza ni nani
amewaroga‭? ‬Imefika hatua nimeona niwaulize swali hilo kutokana na
mustakabali mzima wa mvuto wa sanaa yenu uliopo kwa sasa‭.‬Kutokana na
kazi yangu‭, ‬mbali ya kufanya kwa ukaribu na makundi mengine ya
kijamii‭, ‬nimefanya na nyinyi kwa muda mrefu kidogo‭, ‬najua baadhi
yenu mtakuwa ni mashahidi wa hili‭.‬
Pointi yangu hapa ni hii‭.
‬Kuna wakati nyinyi wasanii wa filamu mlikuwa juu sana kimauzo‭,
‬umaarufu na hata mafanikio kwa jumla‭. ‬Mlikuwa ndiyo mnaozungumzwa
mitaani na kila rika‭. ‬Si watoto‭, ‬mama na hata baba zao‭. ‬Sinema
zilikuwa‭ ‬‮!‬٪zinakamata‮!&‬‭ ‬watu kwelikweli‭.‬
Si mnakumbuka
kipindi kile mlivyokuwa mnaonekana nyinyi tu hata katika muziki wa
bendi‭, ‬watakuwepo mastaa wengi ukumbini lakini‭ ‬utasikia majina ya
wasanii wa Bongo Movies‭ ‬‮!‬٪yakirushwa‮!&‬‭ ‬ukumbini‭. ‬Mitaani
kwenye‭ ‬‮!‬٪vibanda-umiza‮!&‬‭ ‬ilikuwa kila mmoja anazungumzia
mastaa wa sinema pengine kuliko mastaa wa muziki‭, ‬wanasiasa na‭ ‬hata
wanamichezo‭. ‬Lakini kwa takriban miaka mitatu iliyopita ufalme wenu
umepokwa na Bongo Fleva‭.‬
Sasa hivi watoto wanamjua Diamond‭, ‬Ali
Kiba na wengineo lakini si nyinyi tena‭. ‬Wanafuatilia kazi zao‭,
‬wanafuatilia habari zao‭. ‬Wanataka kujua wanafanya nini katika maisha
yao ya sanaa kila siku‭. ‬Mafanikio ya wasanii wa muziki yanaonekana
dhahiri‭. ‬Mashabiki‭ ‬wanaona wanavyovuka mipaka‭, ‬wanaona wanafanya
shoo na kutengeneza mamilioni katika nchi za watu‭.‬
Upande wenu
kimya kimetawala‭. ‬Si kwamba hamtoi muvi‭, ‬la hasha‭. ‬Mnatoa lakini
mvuto umepungua‭. ‬Watu hawazifuatilii sababu mvuto wenu umeshuka‭.
‬Sinema mnazitoa‭, ‬Wabongo hawaoni zile mishemishe za nyinyi kutangaza
kazi mpya‭, ‬kufanya matamasha makubwa ya sinema‭, ‬kuvuka mipaka ya
Tanzania hata kwa kufanya ziara katika nchi za jirani kama ilivyokuwa
kipindi kile cha kina Vincent Kigosi‭ ‬‮!‬٪Ray‮!&‬‭, ‬Steven
Kanumba‭ (‬marehemu‭) ‬na wengineo‭.‬
Ndugu zangu mbona mliweza
kipindi kile halafu sasa mshindwe‭? ‬Hata kama mnashindwa kwenda kwa
pamoja jitihada binafsi zinahitajika‭. ‬Pigeni kazi za‭
‬‮!‬٪individual‭,‬‮!&‬‭ ‬vukeni mipaka kwa nguvu zenu tuone
mnatoboa‭.‬
Msikae mbali na vyombo vya habari‭, ‬mnajiharibia
wenyewe bila kujijua‭. ‬Fanyeni kazi‭, ‬zifikisheni kwenye media kazi
zenu zitangazwe na si kuweka chuki na waandishi halafu baadaye mnakuja
kulaumu kwamba mnatengwa‭.‬
Najua mnaweza‭, ‬naamini mnaweza kuamka
na kufanya mambo makubwa ya kushangaza‭. ‬Fanyeni kweli na sisi tutawapa
sapoti‭! ‬Kutakapokucha
Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.