ALIYEKUWA Kocha wa Yanga, Miguel Gamondi ni miongoni mwa makocha wanaotajwa kukifundisha kikosi cha APR ya Rwanda
msimu ujao, baada ya mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Rwanda kuachana na Mserbia Darko Novic.
.
Gamondi aliyeifundisha Yanga kwa mafanikio, kwa sasa yupo huru baada ya kuachana na Al Nasr ya Libya, ingawa taarifa kutoka Rwanda zinaeleza ni miongoni mwa wanaofuatiliwa kutokana na uwezo alionao.
.
Mbali na Gamondi, makocha wengine ni Miguel Cardoso anayeifundisha Mamelodi Sundowns kwa sasa pamoja na na Nabil Maaloul aliyekuwa USM Alger. APR itakayoshiri- ki Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao, imechukua ubingwa wa Ligi Kuu Rwanda ikiwa na pointi 67.